Katika mechi yake ya kwanza dhidi ya Brazil kikosi hicho kilicheza mchezo bora hatua ambayo ilichochea, runinga ya taifa kuonyesha mechi yao iliyofuatia, kitendo ambacho hakijawahi kufanyika katika historia ya nchi hiyo.
Lakini Korea ilipoteza mechi hiyo baada ya kunyukwa mabao saba kwa bila na Ureno.
Matokeo hayo yalichukuliwa kuwa yameiletea aibu kubwa nchi ya Korea ya Kaskazini.
Madai kwamba kocha wa timu hiyo Kim Jong Hun amehukumiwa kifungo cha kazi ngumu katika ujenzi wa nyumba hayakuweza kuthibitishwa.
Inaelekea hivi sasa FIFA imechochewa na taarifa zaidi kutoka chama cha kandanda cha Korea ya Kusini na imetuma barua kwa Korea ya Kaskazini kama madai hayo ni kweli.

Madai hayo yalijitokeza kwanza katika ripoti ya kituo kimoja cha redio kutokana na mahojiano na mfanyabiashara mmoja wa Kichina ambae inasemekana alikuwa na fungamano na maafisa wa Korea ya Kaskazini.